HABARI

 

Saturday, February 8, 2014

NAPE ALAANI UNYAMA UNAODAIWA KUFANYWA NA CHADEMA

0 Comments

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za CCM Mkoa wa Mwanza.Nape alisema kitendo cha wana CCM kushambuliwa ni kitendo cha kinyama na kinatakiwa kikemewe na kila mtu,pia alisisitiza Vijana wa CCM kuwalinda wapigaji kura wao siku ya kupiga kura.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na waandishi wa Habari kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Mwanza.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitazama picha ya X-Ray  ya Sebastian Masonga Katibu wa UVCCM kata ya Majengo Wilaya ya Kahama,Masonga amevunjika mkono wa kushoto baada ya kupigwa na wafuasi wa Chadema wakati walipokua wanarejea kwenye mikutano ya  kampeni za Udiwani.
Katibu wa NEC Itikadi na uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akimpa pole Afisa Mtendaji wa Kata ya Ubagwe wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ambaye alipigwa na kutobolewa macho na wafuasi wa Chadema .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoka nje ya jengo la hospitali ya Bugando akiongozana na baadhi ya viongozi wa CCM Mkoa wa Mwanza ambapo waliwatembelea na kuwajulia hali majeruhi walioumizwa na wafuasi wa Chadema mjini Kahama.

0 Comments:

Post a Comment